Magazeti ya Jumanne, Januari 18, yameangazia uchaguzi mkuu wa Agosti 9 huku magavana 30 wakimuunga mkono kinara wa Orange Democratic Movement (ODM), Raila Odinga kuingia Ikulu.
Daily Nation
Raila amepigwa jeki na magavana wapatao 30 katika azma yake ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu.
Hatua hiyo inamuweka waziri huyo wa zamani katika nafasi nzuri ya kuzoa kura nyingi za maeneo na vilevile uwezo wa kifedha wa kufadhili kampeni za kitaifa.
Raila aliidhinishwa na magavana hao wakati wa mkutano mjini Naivasha mnamo Jumatatu, Januari 17.
Wakati wa hafla hiyo, gavana wa Makueni, Kivutha Kibwana, alifuta azma yake ya kuwania urais ili kumuunga mkono Raila.
![](https://westernkenyatimes.co.ke/wp-content/uploads/2021/12/IMG-20211218-WA0004.jpg)
Collins Oluyali is a popular columnist who reviews the Kenyan dailies every morning in the Magazetini section, giving it a political angle with facts weaved in rich Kiswahili. Collo is also a strategist in the WKT team.