AFCON: Mane kumenyana na Salah baada ya Senegal, Misri kupenya fainali
Mohamed Salah kumenyana na mwenzake Mane katika fainali ya AFCON [Picha-hisani]

AFCON: Mane kumenyana na Salah baada ya Senegal, Misri kupenya fainali

Ni rasmi sasa kwamba washambulizi Sadio Mane na Mohamed Salah, wote nyota wa timu inayocheza ligi kuu ya Uingereza, Liverpool, watakabana koo katika fainali ya AFCON.

Hapo jana Misri iliingia katika kilele cha mashindano hayo baada ya kuwacharaza wenyeji Cameroon 1-3 katika matuta ya penalti baada ya muda wa kawaida kuishia sare tasa.

Wachezaji wa Misri, wakiongozwa na Mohamed Salah, baada ya kucharaza wenyeji Cameroon kupitia matuta katika mechi ya jana [Picha-hisani]

Senegal walishinda Burkina Faso Jumatano baada ya kuwarindima 3-1 na kujibwaga katika fainali hii ya kukata na shoka ambayo itaandaliwa Jumapili saa nne usiku.

Mechi kusaka mshindi wa tatu na nne, ambayo itakuwa dhidi ya wenyeji Cameroon na Burkina Faso,itachezwa Jumamosi hii saa nne usiku.

Share this article
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *