Magazeti yanaarifu kuwa Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru ameapa kumpa Rais Uhuru Kenyatta funzo la kisiasa ambalo hatathubutu kusahau.
Waiguru anadai eneo la Mlima Kenya lishasonga mbele sasa likiwa chini ya DP Ruto na kuacha mambo ya kizamani ya Uhuru
Waiguru alikuwa mwandani wa Uhuru lakini akaguria UDA ya Ruto mnano Oktoba 2021.
Ijumaa ya Februari 11, magazeti ya Kenya yaliripoti kuhusu siasa za urithi za mwaka 2022 ambapo Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru alidai kuwa chama tawala cha Jubilee ‘kilikufa na kikazikwa’.
Magazeti haya vilevile yanaarifu kuwa mwanafunzi anayekisiwa kuwa nyuma ya moto mkubwa ulioteketeza bweni la shule ya wasichana ya Moi, jijini Naiorbi, atahukumiwa mnano Februari 24.
Daily Nation
Gavana wa Kirinyaga Anne Waigiri ameapa kumpa Rais Uhuru Kenyatta funzo la kisiasa ambalo hatawahi kusahau katika uchaguzi mkuu wa 2022.
Waiguru, mwandani wa zamani wa kiongozi huyo wa taifa, aligura kambi ya Uhuru na kujiunga na UDA ya Ruto mnano Oktoba 2021 kwa kile kinachodaiwa kuwa shinikizo kutoka kwa wapiga kura.
Gavana huyo wa zamani wa Ugatuzi alisisitiza kuwa eneo la Mlima Kenya ambalo linajivunia ukwasi wa kura linaunga mkono azma ya urais ya Ruto na kuongeza kuwa kambi ya Azimio la Umoja inayoongozwa na kinara wa ODM Raila Odinga inarambishwa sakafu peupe katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9.
Collins Oluyali is a popular columnist who reviews the Kenyan dailies every morning in the Magazetini section, giving it a political angle with facts weaved in rich Kiswahili. Collo is also a strategist in the WKT team.