Wafanyibiashara wadogo Bungoma walalamikia ukosefu wa mikopo ya kujiendeleza
Wafanyibiashara mjini Bungoma [Picha-Sam Oduor, WKT]

Wafanyibiashara wadogo Bungoma walalamikia ukosefu wa mikopo ya kujiendeleza

Wafanyibiashara wa kipato cha chini mjini Bungoma wanalalamikia ukosefu wa ufadhili wa mikopo ya kuendeleza biashara zao.

Wakiongozwa na Bi Violet Wakoli, wafanyibiashara hao wanasema imekuwa vigumu kwao kupata mikopo katika mashirika husika mjini humo. Wanadai mashirika hayo hayakubali wafanyibiashara wadogowadogo maana biashara zao ni ndogo mno na inabidi wao kuomba mikopo kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki.

Bi Wakoli anasema biashara zao zinakabiliwa na hatari ya kutoajiri watu wengine kwa kuwa hali ya uchumi ni mbaya.

“Changamoto zingine zinazoathiri wafanyibiashara wadogo ni miundo msingi duni, ukosefu wa rasilimali na ukosefu wa kuwepo kwa serikali kuwasaidia.
Biashara ndogondogo hazifai zidhalalishwe. Zinaweza kuwa uti wa mgongo na kurudisha hadhi ya uchumi wetu ambao umelemazwa na kurudi katika hali yake ya awali. Kwa hivyo, serikali iingilie kati na kufufua biashara hizi,” Bi Wakoli aliongezea.

Share this article
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *