Magazetini: Karua na Mudavadi ndio wanaopendelewa zaidi kama wagombea wenza

Magazetini: Karua na Mudavadi ndio wanaopendelewa zaidi kama wagombea wenza

Karua na Mudavadi wana uungwaji mkono zaidi ya wengine.

Magazeti ya Ijumaa, Mei 13, yanaangazia taarifa kuhusu walio bora katika kuwa wagombea wenza wa Raila Odinga na William Ruto.

Aidha kuna taarifa pia kuhusu kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ikulu Alhamisi Mei 12 ambapo uhusiano baridi uliendelea kushuhudiwa kati ya Rais na naibu wake.

Daily Nation

Gazeti hili linaripoti kuhusu utafiti wake wa ni nani anafaa kuwa mgombea mwenza katika miungano ya Kenya Kwanza na Azimio la Umoja.

Kwa mujibu wa utafiti huo, Martha Karua ndiye anapendelewa zaidi kama mgombea mwenza wa Raila Odinga ndani ya Azimio.

Kwa mujibu wa wafuasi wa muungano huo, asilimia 41 inasema Karua ni kiboko yao huku asilimia 27 ikimuunga mkono kinara wa Wyper Kalonzo Musyoka na kisha Peter Kenneth kwa asilimia 10.

Ndani ya Kenya Kwanza, Musalia Mudavadi ndiye chaguo huku akifuatiwa na Kindiki Kithure na kisha Gavana Ann Waiguru.

Share this article
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *