Magazetini: Aina hatari ya kisonono yatua Nairobi
The Star/Hisani

Magazetini: Aina hatari ya kisonono yatua Nairobi

Aina hiyo mpya ya kisonono hainyoshi dalili miongoni mwa wangonjwa.

Magazeti ya Alhamisi, Januari 12, yameangazia mfumo mpya wa ushuru, na pia mageuzi yaliyopendekezwa na Rais William Ruto katika Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS).

Taifa Leo

Gazeti hili linaripoti kuwa wachungaji watatu walifikishwa katika mahakama ya Eldoret, Jumatano, Januari 11, kwa kumiliki bunduki mbili ya AK47 na risasi nane.

Titus Kipruto, Caleb Nyongesa na Frankline Kipruto waliokamatwa Disemba 2022, walishtakiwa kwa kumiliki bunduki bila leseni.

Watatu hao wanaripotiwa kwamba walipatikana Disemba 2022, na bunduki aina ya AK47 katika kaunti ndogo ya Kapseret bila leseni.

The Star

Kulingana na gazeti la The Star, aina mpya ya ugonjwa wa kisonono umekita kambi jijini Nairobi na kuhatarisha maisha ya wengi.

Wataalamu wameelezea wasiwasi wao huku wakifichua kuwa wakazi wengi wa mijini wanaugua ugonjwa huo ambao unahatarisha sana afya yao ya uzazi.

Matokeo hayo yametokana na utafiti uliofanywa mwaka jana baada ya sampuli kuchukuliwa kutoka kwa kahaba mwenye umri wa miaka 24.

Watafiti walisema kwamba wanaougua ugonjwa huo ni nadra sana konyesha dalili zozote.

Share this article
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *