Magazetini: Mwanafunzi asimulia jinzi alivyokwepa ajali ya basi la Chuo Kikuu cha Pwani
Ukurusa wa mbele wa The Standard/Hisani

Magazetini: Mwanafunzi asimulia jinzi alivyokwepa ajali ya basi la Chuo Kikuu cha Pwani

Ajali ya waliofariki katika ajali sasa imefika 17.

Magazeti ya Ijumaa Machi 31 yanaangazia maandamano ya kiongozi wa Azimio Raila Odinga yaliyogeuka makabiliano kati ya wafuasi wake na polisi.

Aidha, kuna taarifa pia kuhusu ajali iliyohusisha basi la chuo kikuu cha Pwani katika eneo la Kayole Naivasha.

The Standard

Gazeti hili limeripoti kuhusu ajali ya basi la Chuo Kikuu cha Pwani ambalo lilihusika katika ajali eneo la Kayole Naivasha.

Watu 16, na sasa imefika 17, walifariki dunia huku wengine 50 wakibaki na majeraha mabaya na wanapokea matibabu katika hospitali.

Mkuu wa polisi Naivasha, Samuel Waweru, alisema ajali hiyo ilisababishwa na kufeli kwa breki za basi, hali iliyofanya matatu ya abiria 14 kugongwa na basi hilo.

Mwanafunzi kwa jina Brian Safari alisimulia jinsi aliponea ajali hiyo baada ya kuamua kuahirisha kusafiri alipougua.

Share this article
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *