
Man United kumenyana na Chelsea usiku huu/Hisani
Vijana wake Erik Ten Hag wanawakaribisha Chelsea ugani Old Trafford katika mechi ya Ligi Kuu nchini Uingereza leo saa nne usiku.
Man United watajikatia tiketi ya kuingia Champions League iwapo watashinda ama kutoka sare katika mechi hii.
Ushindi dhidi ya Chelsea utaimarisha kampeni yao ya kumaliza nafasi ya tatu mbele ya Newcastle ambao tayari wamefuzu Champions League.
Chelsea nao wanasaka kuboresha matumaini ya mashabiki wao baada ya msururu wa matokeo mabovu.
Katika mechi tano ambazo wamekutana, Mashetani Wekundu na Wanasamawi wametoa sare.
Mechi tatu zimeishia 1-1, mbili 0-0.

Tom Lutali thrives in covering and writing sports fashionably in Kiswahili, a language he has mastered in telling stories in the most elaborate way. A graduate of media studies at the Elgon View College, Tom is a shining star in the media industry.