Police line do not cross yellow tape
[Photo-Courtesy]

Msichana, 21, auawa kinyama akitafuta malisho ya mifugo

Kiini cha tukio hilo bado hakijabainika.

Familia moja Molem katika eneo bunge la Endebess, kaunti ya Trans Nzoia, inalilia haki baada ya mwanao mwenye umri wa miaka 21 kuuawa kinyama katika shamba la mahindi na watu wasiojulikana.

Rose Simiyu, mamake msichana huyo amesema kuwa mwanawe alikuwa akiwatafutia ng’ombe nyasi wakati alipotendewa unyama huo.

“Mtoto wangu wamemgonga vibaya wamemvunja shingo, naomba serikali inisaidie mtoto wangu nipate haki,” mama Rose alilalama.

Kulingana na wakazi, visa vya mauaji vimekithiri eneo hilo huku wakitaka idara za usalama kushika doria.

Share this article
Leave a Comment

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *