
Nahodha wa Sheffield United Billy Sharp [Picha-Hisani]
Nahodha wa Sheffield United, Billy Sharp, aliachwa na majeraha baada ya kushambuliwa na mashabiki kufuatia mchuano wa kufuzu katika daraja ya ligi kuu Uingereza mkondo wa pili dhidi ya Nottingham Forest.
Forest walishinda mchuano huo wa raundi ya pili katika mikiki ya penalti na kughadhabisha mashabiki wa Sheffield ambao waliingia uwanjani baada ya kuona upande wao umelemewa.

Meneja wa Sheffield United, Paul Heckingbottom, alisema baada ya mechi hapo ndipo Sharp alipojeruhiwa.
“Ni unyanyasaji,”alisema Hecklingbottom. “Tumeona mmoja wa wachezaji wetu akivamiwa. Alibebwa juu, alivuja damu, hasira. Itashughulikiwa.”
Akiwa amesimama tisti, Sharp alivamiwa na shabiki aliyekuwa uwanjani. Sharp alilamba sakafu huku shabiki huyo akitoroka.
Staa huyo mwenye umri wa miaka 36 ametoa maoni yake katika mtandao wa kijamii wa Twitter.
“Shabiki mmoja mpumbavu alivuruga kandanda ya usiku huo. Hongera kwa Nottingham Forest kwa ushindi wao na kila la heri katika fainali,” alisema kwa gadhabu.


Support our Journalism
The Western Kenya Times is a digital media platform with more than 500,000 email subscribers and followers across all social media platforms. It was founded in March 2020, in the wake of the COVID-19 pandemic, by a team of young professionals in the media industry.
We have grown to be one of the most reliable, independent, factual, and highly admired digital media platforms in Kenya because of our journalism, which has impacted hundreds of families and enabled children to join school, continue with their studies, and get food.
From the very beginning, we have relied solely on our own resources to sustain this incredible work. However, we firmly believe that our growth potential knows no bounds, and we invite you to be a part of our journey. Your support can help us expand our reach, touch even more lives, and foster a society that thrives on truth, untainted by commercial or political manipulation.
You can support us with as little as Sh100 ($1) through Mpesa number 0721747146 (Lonah Kuya) or PayPal account lugaridaily@gmail.com.
For more information:
Call, WhatsApp, or SMS: +254 762 287 571
Email: westernkenyatimes@gmail.com